Header Ads Widget

KATIBU TAWALA KAHAMA AWASHAURI WATALAAMU WANAPOFUNGA HESABU WAHAKIKISHE WANAJIBU VIZURI HOJA ZOTE.



Katibu tawala wilaya ya Kahama Timothy Ndanya akiongea kwenye kikao cha baraza la madiwani maalum halmashauri ya Msalala.

Na  Kareny  Masasy, Msalala

 KATIBU  tawala wilaya ya Kahama  mkoani Shinyanga  Timothy Ndanya  amewashauri wataalamu  wa halmashauri ya Msalala wanapofunga hesabu za mwisho wa mwaka  wahakikishe  hoja zote zinajibiwa  vizuri ili kuondokana na hati chafu.

Ndanya  ametoa ushauri huo  leo tarehe 29/09/2022 alipokuwa kwenye kikao cha baraza la madiwani maalum  la kufunga mwaka  wa hesabu za serikali  ambao ulianza Agosti 15 hadi  tarehe 30 Septemba 2022 katika halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

“Mkiwa mmejibu hoja zenu zote  vizuri mna uhakika wa kupata hati safi na sasa tumeanza robo ya kwanza  ya mwaka lazima mkusanye mapato ya uhakika kwa malengo mliojiwekea”, amesema  Ndanya.

Makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo Flora Sagasaga amesema kuwa  watahakikisha yote yanasimamiwa vizuri  ili kupata hati safi.

“Tunataka na taasisi zingine kama Ruwasa,Tarura na Tanesco zihakikishe  wanaleta taarifa zao mapema  ili kuzipitia lengo la kununuliwa vishikwambi ni kupata taarifa mapema ila tunakwenda vizuri tushikamane ili kumsaidia Rais wetu”amesema Sagasaga.

 Diwani wa kata ya  Ikinda Matrida Musoma amesema kuwa  wanamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha za miradi mbalimbali nayo imesimamiwa vizuri na wataalamu.

“Taarifa hizi ambazo tumezipitia leo imeonyesha tathimini ya mwaka mzima hivyo tumeona wapi tumeteleza  na tuungane kwa pamoja tusimamie vizuri  zaidi”amesema  diwani Musoma.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Msalala Sekela Ntobi akisoma ajenda ya kikao.

Madiwani wa halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Msalala Flora Sagasaga.
Madiwani wakisikiliza hoja katika kikao cha baraza la madiwani.

Post a Comment

0 Comments