Header Ads Widget

FEDHA ZA TOZO ZA MIAMALA ZAOKOA WANAFUNZI ,WAJAWAZITO NA WATOTO KUTEMBEA UMBALI MREFU HALMASHAURI MSALALA.





Mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga akiwataka wanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Nyawile akiwaeleza wasome kwa bidii baada ya kujengewa vyumba vya madarasa kwa fedha za tozo za miamala.

Na  Kareny  Masasy,

MKUU wa wilaya ya  Kahama mkoani Shinyanga Festo Kiswaga   amesema kuwa fedha za  miamala ya tozo kiasi cha  sh  Millioni 537 .5  kilichopokelewa na halmashauri ya  Msalala kimeweza kujenga miradi kwenye sekta ya afya na  elimu.

Kiswaga amesema hayo leo tarehe 10/09/2022 alipofanya ziara ya kutembelea  miradi hiyo ambayo imekamilika kwa asilimia 100 na  mingine kuanza kufanya kazi.

Moja ya miradi aliyotembelewa ni  shule ya sekondari  Nyawile iliyopo kata ya  Kashishi ambayo imejengwa  vyumba viwili vya madarasa kwa fedha za tozo kiasi cha sh Millioni 25 nakuokoa  wanafunzi kutembelea umbali wa zaidi ya kilomita 20.

Pia Kiswaga ameweza kutembelea kituo cha afya  Mwalugulu  kilichopo kwenye kata  hiyo kilichotumia kiasi  cha shilingi Millioni 500  kwa fedha za tozo ya miamala na ndani ya mwezi huu kitaanza kufanya kazi.

Makamu mkuu wa shule hiyo James Matiku amesema kuwa shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 266  ilianzishwa mwaka 2021  ikiwa na vyumba vya madarasa  viwili vilivyoanzishwa kwa nguvu za wananchi na  sasa vyumba vya madarasa viko tisa vyote vimekamilika.

“Awali walikuwa wakisomea shule ya sekondari  ya kata ya  Bulige nakulazimika wanaoishi maeneo ya kata  ya Kashishi kutembea umbali mrefu nakufikia wengine kutomaliza shule kwa kupata mimba na utoro wa rejareja lakini sasa hali hiyo haipo tena wanapata na muda wa kujisomea”amesema mwalimu Matiku..

Makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo Flora Sagasaga  ambaye ndiye diwani wa kata ya Mwalugulu  amesema kuwa anashukuru kuwepo fedha za tozo  za miamala kwani zimewasaidia kupata kituo cha afya na majengo yote muhimu   walikuwa na Zahanati pekee.

“ Wajawazito na watoto walikuwa wakiteseka kwenda Hopsitali ya manispaa ya Kahama kupata huduma umbali wa kilomita  30 hadi 40 lakini sasa watapata huduma hapa hapa kwani kuna jengo la wagonjwa wa nje (OPD)jengo la mama na mtoto,jengo la upasuaji,jengo la kuchomea taka na maabara”amesema Sagasaga.

Ofisa mipango wa halmashauri ya Msalala Elikare Zabron amesema kuwa wamepokea kiasi cha sh Millioni 537.5 kutoka serikalini  fedha za tozo za miamala na ulifanyika mgawanyo sekta ya afya sh Millioni 500 na sekta ya elimu sh Millioni 37.5

‘Ambapo  sh Millioni 25 zimejenga vyumba vya madarasa viwili Nyawile Sekondari,chumba kimoja sekondari ya Chela  sh Millioni 12.5   na kituo cha afya kimoja cha Mwalugulu kiasi cha sh Millioni 500”amesema Zabron.


Chumba cha darasa kilichojengwa kikiwa kimekamilka na wanafunzi wameanza kusomea.


Wanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Nyawile iliyopo kata ya Kashishi halmashauri ya Msalala wakiwa darasani.
Ujenzi ukiendelea wa kituo cha afya kilichopo kata ya Mwalugulu kwa jengo la mama na mtoto..

Jengo la wagonjwa wagonjwa wa nje OPD katika kituo cha afya Mwalugulu.

Post a Comment

0 Comments