
MKUU wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga akizungumza kwenye mkutano mkuu wa chama cha walimu Tanzania CWT wilayani Kahama mkoani Shinyanga
Na  Kareny 
Masasy,  Kahama 
Mkuu  wa wilaya ya Kahama   mkoani
Shinyanga Festo Kiswaga  ametoa maelekezo
kwa  maafisa utumishi wa halmashauri   kuhakikisha wanafuata utaratibu wa
kuwahisha  taarifa za watumishi
wanaokaribia kustaafu na wale wanaotarajia kupanda madaraja kazini  ili kuondoa ucheleweshaji wa stahiki zao.
Kiswaga
amesema hayo  leo tarehe 23/09/2022  alipokuwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa
chama cha walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ulio wakutanisha
wajumbe takribani 250.
Kiswaga
amesema amewapongeza walimu kwa kazi kubwa wanayoifanya ingawa kulikuwa na
changamoto ya mazingira ya kuishi wa walimu serikali  ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia
Suluhu imeanza kuyafanyia kazi na hata waliopandishwa madaraja  wanalipwa stahiki zao .
Kiswaga
amesema kuwa serikali ya awamu ya sita imetekeleza kwa kiasi kikubwa matakwa ya
walimu na kutoa maelekezo  ikiwa  maafisa utumishi wanatakiwa  kuangalia wale wote wenye kukaribia
kustaafu  kuwaandalia nyaraka zao mapema
ili kuondoa kero.
“Nimeambiwa
kuna watu  ambao wako halmashauri ambao
wamekuwa wakichelewesha  kuwapandisha
madaraja walimu sasa tunashughulika nao nakuchunguza kwanini wanachelewesha nanyi
walimu mkiwa na shida  msikae kwenye
mabenchi kusubiri bali mpite moja kwa moja msikilizwe  muwahi 
kufundisha wanafunzi wetu”amesema Kiswaga.
Mwenyekiti
wa  CWT mkoa wa Shinyanga  Mathias  
Balele amesema  kuwa serikali
imefanya kazi kubwa kwa walimu kwani imeweza kuwajengea nyumba na mazingira ya
kufundishia kuwa mazuri huku upandishaji wa madaraja ukienda vizuri tofauti na
zamani.
Mwenyekiti
wa  CWT wilaya ya Kahama  Raymond Lutemba  akiongoza mkutano huo kupitia taarifa ya
utendaji kazi kwa chama hicho kwa kipindi cha miaka miwili na nusu (March 2020 –
Septemba 2022) nakueleza kero mbalimbali wamezitatua ikiwemo uhamisho wa walimu
na wale bado mazungumzo  yanaendelea na
waajiri wao.
 Pia kulikuwa na  ajenda ya 
kuondokana na usafiri wa gari aina ya Coaster iliyokuwa ikibeba abira
25  hali ambayo walieleza inawapa
changamoto katika suala la usafirishaji 
na kuwa bovu mara kwa mara.
Ambapo wajumbe wa mkutano huo walipendekeza kununuliwe gari aina ya TATA itakayobeba abiria 40 itakayosaidia katika kuwasafirisha wao wanapokuwa na shughuli mbalimbali .
 Wajumbe wa mkutano mkuu wa CWT wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga wakisimama tayari kumpokea mgeni rasmi katika mkutano huo.
Wajumbe wa mkutano mkuu wa CWT wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga wakisimama tayari kumpokea mgeni rasmi katika mkutano huo. Wajumbe wa mkutano mkuu wa CWT wilaya ya Kahama wakiwa katika sala kabla ya mkutano kuanza
Wajumbe wa mkutano mkuu wa CWT wilaya ya Kahama wakiwa katika sala kabla ya mkutano kuanza  Wageni waalikwa katika mkutano mkuu wa CWT wilaya ya Kahama wakiwa meza kuu
Wageni waalikwa katika mkutano mkuu wa CWT wilaya ya Kahama wakiwa meza kuu Katibu  CWT wilaya ya Kahama  Peter Gedi akitoa utangulizi katika mkutano mkuu wa chama hicho.
Katibu  CWT wilaya ya Kahama  Peter Gedi akitoa utangulizi katika mkutano mkuu wa chama hicho. Mweyekiti wa CWT mkoa wa Shinyanga Mathias Balele akisalimiana na wajumbe wa mkutano mkuu wilaya ya Kahama
Mweyekiti wa CWT mkoa wa Shinyanga Mathias Balele akisalimiana na wajumbe wa mkutano mkuu wilaya ya Kahama 
Wajumbe wa mkutano mkuu wa CWT wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga

Wajumbe wa mkutano mkuu wa CWT wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga

wageni waalikwa wakiwa meza kuu ni mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga kushoto katikati ni Mwenyekiti wa CWT mkoa wa Shinyanga Mathias Balele na upande wa kushoto ni kaimu katibu wa CWT mkoa wa Shinyanga Allen Shuri
 Wajumbe wa kamati tendaji ya CWT mkoa wa Shinyanga
Wajumbe wa kamati tendaji ya CWT mkoa wa Shinyanga Mwenyekiti wa CWT wilaya ya Kahama Raymond Lutemba akiongea kwenye mkutano
Mwenyekiti wa CWT wilaya ya Kahama Raymond Lutemba akiongea kwenye mkutano Katibu wa CWT halmashauri ya Ushetu Alponnce Mbasa mgeni mwalikwa akisalimia wajumbe wa mkutano mkuu
Katibu wa CWT halmashauri ya Ushetu Alponnce Mbasa mgeni mwalikwa akisalimia wajumbe wa mkutano mkuu 
Mwenyekiti wa CWT halmashauri ya Ushetu akisalimiana na wajumbe wa mkutano mkuu alipoalikwa CWT wilaya ya Kahama.

DK Baraka .C ,Kulwa Mkurugenzi wa hospitali ya CKM iliyopo Runzewe wilaya ya Bukombe mkoani Geita akiwa mdau wa elimu akihudhuria mkutano mkuu kwa kutoa salamu zake.
 
 
       
 
 
