Header Ads Widget

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WANANCHI YAFUTA TOZO


Hatimaye Serikali imesikia kilio cha Watanzania kwa kufuta na kupunguza kiwango cha tozo za miamala ya kieletroniki.

Uamuzi huo umetangazwa leo Jumanne Septemba 20, 2022 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba bungeni baada ya kipindi cha maswali na majibu.

Amesema Serikali imepunguza wigo wa tozo, kuchochea matumizi ya miamala kwa ajili ya kupunguza fedha taslimu, kurahisisha utozaji na kuzuia kutoza tozo husika mara mbili.

“Marekebisho yaliyofanyika ni kufuta tozo ya kuhamisha fedha kutoka benki kwenda mitandao ya simu (pande zote) na kufuta tozo ya kuhamisha fedha ndani ya benki moja (pande zote),”amesema.

Dk Mwigulu ametaja marekebisho mengine ni kufuta tozo ya kuhamisha fedha kutoka benki moja kwenda benki nyingine (pande zote).

Amesema pia wafanyabiashara (merchants) hawatahusishwa kama ilivyo kwenye kanuni za sasa.


Amesema pia wamesamehe tozo ya miamala kwenye utoaji wa fedha taslimu kupitia wakala wa benki na ATM kwa miamala yenye thamani isiyozidi Sh30,000.
 
SOMA HAPA ZAIDI CHANZO MWANANCHI.



Post a Comment

0 Comments