Header Ads Widget

SHANGWE ZATAWALA STENDI YA HIACE SOKO KUU SHINYANGA IKIZINDULIWA

 
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko (katikati) akikata Utepe kuzindua Stendi ya Hiace, Bajaji na Bodaboda iliyopo Soko kuu Manispaa ya Shinyanga, (kulia) Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Getruda Gisema, (kushoto) Diwani wa Chibe John Kisandu.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

WAFANYABIASHARA wa usafirishaji katika Stendi ya Hiace, Bajaji na Bodaboda iliyopo Soko kuu Manispaa ya Shinyanga, wameipongeza Serikali kwa kuifanyia ukarabati Stendi hiyo, na kuwaboreshea mazingira mazuri ya kufanya biashara zao.


Stendi hiyo imezinduliwa leo Agost 16, 2022, ambapo awali ilikuwa ikikabiliwa na uchakavu wa miundombinu, lakini Serikali ikaifanyia ukarabati kuanzia June mwaka huu, na imekamilika Agost na sasa imeanza kutumika Rasmi na imegharimu Sh.milioni 147.

Mmoja wa Wafanyabiashara hao Paschal Mboje, amesema awali Stendi hiyo ilikuwa na vumbi na kipindi cha mvua tope linakuwa jingi na maji kutwama, lakini sasa hivi changamoto hizo hazipo tena na watafanyabiashara zao katika mazingira mazuri.

“Tunaipongeza Serikali kwa kuikarabati Stendi hii, na kutatua Changamoto ambazo tulikuwa tukikabiliana nazo za uchakavu wa miundombinu na tutafanya biashara zetu kwa raha mstarehe,”amesema Mboje.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko, amewataka wafanyabiashara hao waitunze miundombinu ya Stendi hiyo ili waendelee kufanyabiashara zao katika mazingira rafiki.


Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akizungumza mara baada ya kumaliza kuzindua Stendi ya Hiace, Bajaji na Bodaboda iliyopo Soku kuu Manispaa ya Shinyanga.

Mfanyabiashara wa usafirishaji Paschal Makoye akizungumza mara baada ya kumaliza kuzinduliwa Stendi hiyo.

Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko (katikati) akikata Utepe kuzindua Stendi ya Hiace, Bajaji na Bodaboda iliyopo Soko kuu Manispaa ya Shinyanga, (kulia) Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Getruda Gisema, (kushoto) Diwani wa Chibe John Kisandu.

Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko (katikati) akikata Utepe kuzindua Stendi ya Hiace, Bajaji na Bodaboda iliyopo Soko kuu Manispaa ya Shinyanga, (kulia) Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Getruda Gisema, (kushoto) Diwani wa Chibe John Kisandu.
Madereva wa Bodaboda wakiingia kwenye Stendi hiyo.

Madereva wa Bajaji wakiingia kwenye Stendi hiyo.

Hiace zikiingia ndani ya Stendi hiyo.

Hiace zikiingia ndani ya Stendi hiyo.

Hiace zikiwa ndani ya Stendi.

Bajaji zikiwa ndani ya Stendi.

Post a Comment

0 Comments