Header Ads Widget

UKAMATAJI WATU KIMYA KIMYA WAZUA UTATA



Utaratibu wa karibuni wa Jeshi la Polisi kukamata watu kimya kimya na kuwaacha ndugu na jamaa wa waliokamatwa wakihangaika vituoni kuwatafuta umewaibua wadau wa sheria na haki za binadamu wakitaka jeshi hilo kuzingatia sheria na kanuni za ukamataji.



Hoja hizo zimeibuka baada ya polisi kumkamata mratibu wa uhamasishaji wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), Twaha Mwaipaya, kabla ya kumwachia kwa dhamana baada ya siku tano huku ndugu na wanachama wenzake wakihangaika vituoni Dodoma, Morogoro na Dar es Salaam bila kuelezwa mahali alipo.

Hali kama hiyo imeshajitokeza kwa watuhumiwa kadhaa, wakiwemo Erick Kabendera, Mdude Nyagali, Peter Madereka, Freeman Mbowe na wengineo ambao awali polisi walikana kuwashikilia, lakini baadaye wakaonekana walikuwa mikononi mwa Jeshi hilo.

SOMA HAPA ZAIDI CHANZO MWANANCHI.


Post a Comment

0 Comments