Header Ads Widget

MCHOMOKO WATEKETEZA MAISHA YA WATU WATANO SIMIYU, 11 WAJERUHIWA


Watu watano wamefariki dunia na wengine 11 wamejeruhiwa katika ajali ya gari maarufu (Mchomoko) iliyotokea eneo la Magereza nje kidogo ya mji wa Bariadi Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu usiku wa kuamkia leo Julai 13, 2022.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa Simiyu, Blasius Chatanda amesema kuwa ajali hiyo imehusisha magari madogo ya abiria.

"Nimefika eneo la ajali nimeona waliofariki wote ni wanaume. Gari moja mchomoko lilikuwa likitokea Lamadi na lingine Bariadi. Dereva aliyekuwa akitoka Lamadi aliova-take ndipo akakutana na mwenzake. Chanzo ni mwendo kasi. Madereva wamejeruhiwa na wapo chini ya ulinzi,"amesema

Post a Comment

0 Comments