Header Ads Widget

UTPC YAKUTANA NA WAANDISHI WA HABARI WA MITANDAO YA KIJAMII KUPITIA NA KUTHIBITISHA KANUNI ZA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI MTANDAONI

 


Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini Tanzania (UTPC), Abubakar Karsan (kushoto) akifungua Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini Tanzania (UTPC) umekutana na Waandishi wa Habari Mtandaoni (Bloggers/Youtubers) kwa ajili ya kupitia na kuthibitisha Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni na Vyombo vya Habari vya kawaida.

Mkutano huo umefanyika leo Ijumaa Juni 17,2022 katika ukumbi wa Adden Palace Jijini Mwanza na kuhudhuriwa na waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii kutoka mikoa mbalimbali.

Akifungua Mkutano huo, Mkurugenzi wa UTPC, Abubakar Karsan amesema Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni zitasaidia kupunguza wimbi la habari za uongo mtandaoni hivyo kupunguza malalamiko mbalimbali.

“UTPC kwa kushirikiana na IMS ilianza mchakato wa kutengeneza kanuni za maadili ya uandishi wa habari kwa waandishi wa habari wanaofanya kazi kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo magazeti,redio na Televisheni. Mchakato huu ulifanywa na Mama Pili Mtambalike ambapo maoni ya kutengeneza kanuni hizi yalichukuliwa katika Klabu 8 za waandishi wa habari ambazo ni Dar es salaam, Dodoma, Arusha, Iringa, Zanzibar, Mtwara, Kigoma na Mwanza”,amesema Karsan.

Karsan amesema waandishi wa habari za mitandaoni wanapaswa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari kwa kuepuka kuandika habari za uongo, habari potofu na habari chonganishi.

Karsan ametumia fursa hiyo kuwataka waandishi wa habari za mitandao ya kijamii kuwa mabalozi wazuri kuhamasisha wananchi kupata chanjo ya UVIKO – 19 pamoja na kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika Agosti 23,2022.

Kwa upande wake na Afisa Programu wa UTPC, Victor Maleko ambaye ni Mratibu wa Mradi wa Ushirikiano kati ya UTPC na International Media Support (IMS) amesema mitandao ya kijamii imekuwa chanzo kikuu na cha haraka cha habari hivyo ni vyema waandishi wa habari wa mitandao ya kijamii wakaongozwa na Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni ndiyo maana UTPC imeamua kubeba jukumu hilo la kuandaa kanuni hizo.


Naye Mshauri Mwelekezi wa Kutengeneza Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni, Pili Mtambalike amesema maadili ya uandishi wa habari yanafanya mwandishi wa habari au chombo cha habari kuaminika hivyo kuwasihi waandishi wa habari kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini Tanzania (UTPC), Abubakar Karsan (kushoto) akifungua Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni leo Jijini Mwanza. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini Tanzania (UTPC), Abubakar Karsan (kushoto) akifungua Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini Tanzania (UTPC), Abubakar Karsan (kushoto) akifungua Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.
Afisa Programu wa UTPC, Victor Maleko ambaye ni Mratibu wa Mradi wa Ushirikiano kati ya UTPC na International Media Support (IMS) akizungumza kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.
Afisa Programu wa UTPC, Victor Maleko ambaye ni Mratibu wa Mradi wa Ushirikiano kati ya UTPC na International Media Support (IMS) akizungumza kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.
Afisa Programu wa UTPC, Victor Maleko ambaye ni Mratibu wa Mradi wa Ushirikiano kati ya UTPC na International Media Support (IMS) akizungumza kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.
Mshauri Mwelekezi wa Kutengeneza Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni, Pili Mtambalike akizungumza kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.
Mshauri Mwelekezi wa Kutengeneza Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni, Pili Mtambalike akizungumza kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.
Mshauri Mwelekezi wa Kutengeneza Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni, Pili Mtambalike akizungumza kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakipitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakipitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakipitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 

Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.

Post a Comment

0 Comments