Header Ads Widget

SABABU HIZI HAPA BUNGE KUAHIRISHWA LEO NDANI YA DAKIKA 30

Mwenyekiti wa Bunge, David Kihenzile leo Alhamisi Juni 2, 2022 ameahirisha shughuli za bunge kwa muda wa dakika 30 kwa sababu Waziri wa Nishati, January Makamba na naibu wake, Stephen Byabato hawapo katika ukumbi wa Bunge wakati mjadala wa hotuba ya wizara hiyo ukitaka kuanza.

Baada ya kipindi cha maswali na majibu bungeni leo wabunge walianza kuchangia hotuba ya Wizara hiyo kwa bajeti ya mwaka 2022/23.

Hata hivyo baada ya Kihenzile kumuita mchangiaji wa kwanza Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Catherine Magige, Waziri Januari Makamba na Naibu wake Stephen Byabato hawakuwepo ndani ya ukumbi wa bunge.
 
SOMA ZAIDI HAPA CHANZO MWANANCHI.

Post a Comment

0 Comments