Header Ads Widget

WATU WAWILI MBARONI KWA TUHUMA ZA KUMLAWITI MTOTO WA DARASA LA SITA SHINYANGA

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga George Kyando


Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Watu wawili mmoja mwenye umri wa Miaka 42 na mwingine umri wa Miaka 36 wanashikiliwa na jeshi la Polisi kwa tuhuma za kulawiti mtoto wa darasa la sita mwenye umri wa Miaka 14, wakazi wa Manispaa ya Shinyanga.

Tukio hilo limetokea kwenye mtaa wa Luhende kata ya Masekelo Mkoani Shinyanga ambapo Mwenyekiti wa Mtaa wa Luhende bwana Msafiri Nadula akizungumza na vyombo vya habari ameeleza namna alivyopokea taarifa huku akisema alifika na kuzungumza na mtoto huyo ambaye aliwataja watu hao na tayari wameshikiliwa na jeshi la Polisi.

Mwenyekiti Nadula amesema watuhumiwa hao mmoja ni Baba mwenye nyumba pale familia ya mtoto huyo wamepanga, huku mwenyekiti akisema wameshirikiana na Polisi wa kata ya Masekelo kuwapa watuhumiwa hao.

” Nilipewa taarifa za mtoto huyo kuwa anarudi nyumbani saa saba usiku tarehe 3, Mwenzi huu nilifika nyumbani nikazungumza na mtoto huyo nikamuonya akasema nimekuelewa mwenyekiti sitorudia tena lakini siku iliyofuata nikapigiwa simu saa tano kuwa mtoto huyo ametoka tena “

“Basi asubuhi nikaenda tena nyumbani kwao nikamkuta bado amelala ikabidi nimchukue huyo mtoto ili nijue ni changamoto gani anazokutana nazo hadi kuingia nyumbani saa saba usiku akaniambia mama anashinda kwenye vilabu vya pombe nikamuuliza wewe huwa unaenda wapi usiku akasema kwamba tunaenda kutembea kwa mwarabu siku ya sikukuu alitupa Shilingi Miasaba (700)”

“Nikaendelea kumhoji akawa anabishabisha lakini badae akasema sawa mimi nilifundishwa na dada yangu huyo mwarabu ni hawala wangu basi nikampeleka kwa mtendaji tukaendelea kumhoji akakubali yote hayo kwamba huyo mwarabu ni hawala yake ameshafanyanaye mapenzi zaidi ya mara tatu, akasema na baba mwenye nyumba huwa natoka naye alinikuta usiku nimelala akanilazimisha kufanya mapenzi lakini mama anajua aliniambia niendelee kufanya mapenzi na baba mwenye nyumba ili nikikua anioe”.

Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishina msaidizi wa Polisi George Kyando amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema jeshi hilo limewakamata watuhumiwa huku likiendelea na uchunguzi zaidi ili hatua za kisheria zichukuliwa. 
 
“Ni kweli tukio hilo limetokea kwamba mtoto wa Miaka 14 ni binti mwanafunzi wam darasa la sita (6) alikuwa akilawitiwa na watu wawili mmoja mwenye umri wa Miaka 42 na mwengine anaumri wa Miaka 36 inaonekana tende hilo nila muda mrefu lilikuwa halijagundulika lakini mpaka sasa tayari watuhumiwa hao wawili wote tumeshawakamata na uchunguzi unaendelea na upelelezi ukishakamilika hatua za kuwafikisha mahakamani zitafanyika” amesema kamanda Kyando

Post a Comment

0 Comments