Header Ads Widget

NAIBU WAZIRI KATAMBI ABAINISHA KIASI CHA SH. BILIONI 150 ZIMETOLEWA MIKOPO KWA VIJANA, AMBAYE HAJAPATA MKOPO HUO HUENDA NI MKENYA

NAIBU Waziri wa Vijana, Kazi na Ajira, Patrobas Katambi amesema vijana wote wamepata mikopo kupitia halmashauri na ambaye hajapata huenda ni Mkenya.

Katambi amesema hayo leo Mei 18, 2022 bungeni mjini Dodoma, akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Sophia Mwakagenda, aliyehoji vijana kutopata ajira kwa zaidi ya miaka sita sasa pamoja na kwamba kuna mfumo wa utoaji wa mikopo katika halmashauri , hivyo mfumo huo unawatupa nje.

“Ukiangalia hakuna kijana yeyote ambaye hapati mkopo, kumekuwa na scheme za utoaji mkopo katika elimu, sekondari tumekuwa tukitoa elimu bila malipo, chuo kikuu anakutana na Bodi ya Mikopo, akitoka chuo akienda kwenye halmashauri zetu tunatoa mikopo.

“Pia tumekuwa na scheme za makubaliano na mabenki mbalimbali kushusha riba na kutoa mikopo, kama mtapitisha bajeti ya Wizara ya Kilimo, kule kuna mpango wa 'Building the better tomorrow' utakaogusa zaidi ya vijana milioni 1, ili kutengenezewa scheme za kilimo,” amesema.

Hata hivyo kauli hiyo ilipingwa na Mwakagenda, ambaye alisema: “Mhe. Naibu Waziri (Katambi), unavyoeleza ni kama vile uko nje ya Tanzania, tuna vijana wengi sana wamekosa ajira zaidi ya miaka sita sasa, umesema kwenye halmashauri kuna nafasi za wao kupata pesa, vijana wengi mfumo unawaacha nje.”

Katika swali la nyongeza Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina alihoji ni kwa nini serikali isiandae mfumo mzuri wa kuwakopesha vijana wasiokuwa na ajira wale wanaotaka kuingia kwenye ujasiriamali wakakopeshwa hata walau mtaji wa Sh Milioni 20 wa kuanzia na wakajidhamini kwa vyeti vyao vya chuo

Akijibu swali hilo, Katambi alisema zaidi ya Sh bilioni 150, zimekwishatolewa kwa vijana kama mikopo na kama kuna kijana yeyote ambaye hajapata mkopo itakuwa pengine ni Mkenya.

SOMA ZAIDI HAPA CHANZO HABARI LEO.

Post a Comment

0 Comments