Header Ads Widget

POLISI WADAIWA KUMUUA MUUZA MADINI NA KUCHUKUA SHILINGI MILIONI 70

Maofisa saba wa Jeshi la Polisi, wanashikiliwa na jeshi hilo mkoani Mtwara kwa tuhuma za kumpora mfanyabiashara mmoja wa madini Sh70 milioni na kisha kudaiwa kumuua kwa kumchoma kwa sindano ya sumu na kuutupa mwili wake baharini.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Mark Njera alisema jana kuwa tukio la mauaji lilitokea Januari 5 baada ya Hamis (Mussa) kufuatilia fedha zake zilizochukuliwa na maofisa wa polisi.

Alisema maofisa hao walikwenda kumpekua hapo lodge, zilipatikana Sh2.3 milioni, lakini katika mahojiano alieleza kuwa hizo fedha alikuwa akifanya kazi zake Dar es Salaam na marafiki zake walifanya tukio huko wakapata fedha hizo.
 
SOMA ZAIDI HAPA CHANZO MWANANCHI.

Post a Comment

0 Comments