Header Ads Widget

KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA YAFANYA ZIARA KUJIONEA MIRADI INAYOTEKELEZWA NA FEDHA ZA UVIKO-19.




Kamayti ya siasa ikijadiliana baada ya ukaguzi wa ujenzi wa maabara katika shule ya Mwadau sekondari.


Wajumbe wa kamati ya siasa ya CCM wakipatiwa maelekezo juu ya ujenzi wa Jengo la maabara Wkatika shule ya sekondari ya Mwadui Technical iliyopo Kishapu

Na  Kareny  Masasy

KAMATI ya siasa  ya chama cha Mapinduzi  (CCM) mkoa wa Shinyanga   imerizishwa na  baadhi ya miradi ya sekta ya elimu na afya  inayotekelezwa kwa  fedha za uviko -19  wilayani Kishapu.

kamati  hiyo   ikiongozwa na mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi  (CCM) Mabala Mlolwa  na  walifanya ziara jana  ya kukagua ujenzi wa majengo  ya  wagonjwa wa n je OPD,Maabara na kichomea taka katika  kituo cha afya kilichopo kijiji cha Negezi  kata ya Ukenyenge kilichofikia asilimia 51 katika ujenzi wake,

 "Ni suala la kumpongeza Rais  Samia Suluhu sababu amehangaika kuzitafuta fedha ili kuhakikisha wanafunzi hawakai kwenye mrundikano  tena wala chini  na madarasa kuibuka kama uyoga kweli ametekeleza ilani ya chama kwa vitendo katika sekta ya elimu"amesema  Mlolwa..

Mkuu wa wilaya ya Kishapu  Joseph  Mkude amesema  kuwa shule  ya sekondari zipo 32  ambapo walipokea kiasi cha sh Billioni moja kwaajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 97 ikiwa vyumba 81 vya shule ya sekondari na  madarasa 16 kwenye  shule shikizi  na ujenzi  umekamilika kwa asilimia 96.

Mkunde amesema kuwa kila siku wanapiga hatua  katika kutekeleza miradi mbalimbali   na  pamoja na madawati  yote na ofisi za walimu   ambapo walitarajia kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza jumla ya wanafunzi  4456.

Mkuu wa shule ya sekondari  Shinyanga (shybush)  Bernard Ishengoma  alisema kuwa  walipewa kiasi cha sh Millioni 40 katika shule hiyo nakuweza  kujenga  vyumba vya madarasa  mawili  na madawati 80 kila darasa na ofisi moja jumla kunakuwa na vyumba vya madarasa 23.

Mkuu wa shule ya sekondari Kishapu  Kaji Kapyen amesema kuwa  vyumba vya madarasa vimekamilika vyote  na wanafunzi 195 walipangiwa shule hiyo  kutokana na  takwimu hiyo na kuwepo madawati na vyumba vya madarasa   hakuna mrundikano  wa wanafunzi hata wakiripoti wote.





Post a Comment

0 Comments