Header Ads Widget

SAMIA SULUHU HASSAN AAPISHWA KUWA RAIS WA 6 TANZANIA


Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiapa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Machi 19, 2021 katika Ikuru ya Magogoni Mkoa wa Dar es Salaam. Ameapishwa leo baada ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kufariki Dunia Machi 17, 2021.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ameapishwa kuwa Rais wa sita wa Tanzania na Jaji Ibrahim Juma katika Ikulu ya Jijini Dar es Salaam.

Hafla ya kuapishwa kwake imefanyika Ikulu Dar es Salaam na kuweka historia ya kuwa Rais wa kwanza mwanamke nchini Tanzania.

Samia amechukua nafasi ya aliyekuwa rais wa Tanzania, John Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, 2021 kwa maradhi ya moyo katika hospitali ya Mzena jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Post a Comment

0 Comments