Header Ads Widget

JUMUIYA YA WAZEE WILAYA YA SHINYANGA VIJIJINI YAADHIMISHA KWA KUPANDA MITI NA KUTEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO MWALUKWA

 

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga Vijijini Bi Ernestina Richard akipada mti katika shule ya Msingi Bulambila kata ya Mwalukwa, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 44 ya (CCM).

Katika kuelekea Maadhimisho ya Miaka 44 ya  kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini hapo February 5 Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Shinyanga Mjini imeadhimisha kwa kufanya shughuli za kijamii ikiwemo kupanda miti katika eneo la Shule ya Msingi Bulambila na Sekondari ya Mwalukwa katika kata ya Mwalukwa.

Akiongoza zoezi la Upandaji miti Katibu wa (CCM)  Wilaya ya Shinyanga Vijijini Bi Ernestina Richard amesema kuwa miaka 44 ya chama cha Mapinduzi nchini  wanajivunia mafanikio makubwa katika Nyanja mbalimbali ikiwemo uboreshaji wa sekta ya Afya,Elimu Miundombinu ya Barabara, Umeme Vijijini na Maji.

Ernestina amesema Chama Cha Mapinduzi kimeweza kuleta mageuzi Makubwa nchini ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo hali ilikuwa tofauti na miaka ya hivi karibuni kwani kiwango cha hali ya uchumi ilikuwa kawaida sana ambapo  sasa taifa linakimbia.

Aidha ameongeza kuwa maadhimisho ya mwaka huu yameadhimishwa kwa mfumo tofauti kwa kufanya kazi za kijamii kwani jumuiya ya wazazi inayo jukumu la kukuza maadili na umuhimu wa utunzaji wa mazingira ndo maana wameamua kuadhimisha kwa kupanda miti ambayo ni zaidi ya 1000

Bi Ernestina amebainisha kuwa  chama chake kitaendelea kusimamia utekelezaji wa ilani  kwa kuhakikisha miundombinu ya elimu,elimu, maji na mengine inaimarika ambapo maadhimisho hayo yanayawakumbusha kufuatilia utekelezaji wa ilani ambayo imebainishwa kitabu cha ilani ya 2020-2025 ili iweze kufikiwa vizuri

Akieleza ahadi za Mheshimiwa mbunge wa Jimbo hilo Ahmed Salum ambaye amepata dharura amesema kuwa mbunge huyo ametoa ahadi ya mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ukamalishaji wa ujenzi wa matundu ya Vyoo 14  katika shule ya Msingi Bulambila ambayo yameanza kujengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na  mifuko 50 kwa ajili ya  ujenzi wa zahabnati ya kijiji cha Ng”ang”a

Katibu huyo amewaongza wananchi kwa ushiriki wao mzuri kwenye miradi ya maendeleo kwa kujitoa katika michango mbalimbali ikiwemo ujenzi wa madarasa,matundu ya vyoo  na zahanati.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Wilaya ya Shinyanga Vijijini Peter Kawiza amesema kuwa wao kama jumuiya ya wazazi wameamua kuadhimisha kwa kufanya shughuli za kijamii ambapo ameeleza kuwa suala la changamoto zilizopo kwenye jamii bado zinaendlea kufanyiwa kazi kwani serikali imeendelea kufanya vizuri kwa kutatua kero za wananchi

Mheshimiwa Peter amesema kuwa licha ya uwepo wa baadhi ya changamoto katika jamii lakini chama na serikali kwa pamoja wanaendelea kupambana kutatua kero hizo

Ameongeza kuwa jumuiya uandaa watu katika hatua mbalimbali ikiwemo malezi, elimu na kua viongozi wazuri wa baadaae amabao watakuja kulitumikia taifa ili iwe na vijana wazuri waloandaliwa  kwa uzuri

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga vijijini ambaye pia ni diwani wa kata ya Mwalukwa Bw. Ngasa Mboje amesema kuwa serikali ya chama cha mapinduzi inaendelea na utatuzi wa changamoto zinazowakabili wananchi  wa kata ya Mwalukwa ikiwemo  uhaba wa Maji na umeme kwa baadhi ya vijijini ambavyo havijapata umeme.

Ngassa amesema kuwa shughuli nyingi zinazofanywa katika Kata yake zinafaywa kwa nguvu za wananchi ikiwemo michango mbalimbali ikiwemo ujenzi wa madarasa ambapo hadi sasa wamejenga madarasa mawili katika shule ya sekondari Mwalukwa ambapo kila kaya ilikuwa ikichanga kiasi cha Shilingi elfu ishirini na moja.

Naye katibu wa Jumuiya  ya wazazi wilaya ya Shinyanga Vijijini Abdalah Kilobi ameitaka jamii kuhakikisha  inawalea watoto katika maadili  yampasayo ili kujenga jamii iliyositarabika na yenye kuwa na matunda mazuri kwa taifa lijalo.

Nao baadhi ya wachama wa chama cha mapinduzi (CCM) kata ya Mwalukwa wamepongeza kuadhimisha  miaka 44 ya (CCM)  kutokana na mabadiliko makubwa yaliyofanywa na chama hicho hapa nchini ikiwemo ukuaji wa uchumi toka uchumi wa chini hadi kati, uboresheaji wa miundombinu mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Reli ya Kisasa na upelekaji wa umeme vijijini.

Maadhimisho ya  Chama cha Mapinduzi  ufanyika kila mwaka ifikapo mwezi February tarehe 5.


Wanachama wa Chama cha Mapiduzi-(CCM) kata ya Mwalukwa na Jumuiya ya Wazazi  Wilaya ya Shinyanga vijijini wakitekeleza zoezi la upandaji miti kuadhimisha miaka 44 ya (CCM) 

Wakazi wa Mwalukwa wakiwasikiliza Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi Shinyanga Vijijini waliofika kuadhimisha miaka 44 ya (CCM)

Wajumbe wa Jumuiya ya Wazazi wakiendelea  na ukaguzi wa Miundombinu ya Madarasa Shule ya Sekondari Mwalukwa 
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Ngassa Mboje akichimba shimo kwa ajili ya kupanda miti Shule ya  Msingi Bulambila kata ya Mwalukwa 

Mwenezi wa CCM Wilaya ya Shinyanga Vijijini Bw Emanuel akiendelea na zoezi la uchimbaji wa mashimo 



Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Wilaya ya Shinyanga Vijijini Peter Kawiza akipanda mti 

\





































Post a Comment

0 Comments