Header Ads Widget

MKURUGENZI MKUU TBS AGUSWA NA UTENDAJI IDARA KUU YA MAENDELEO YA JAMII



Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango nchini, TBS Dkt.Athuman Ngenya (kulia) akiangalia majarida na vitabu mbalimbali vya miongozo inayotokewa na Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii wakati aipotembelea banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya Nanenanekatika viwanja vya Nyakabindi, Simiyu. Kushoto ni Afisa Ustawi wa Jamii Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Loata Mollel.

Na Mwandishi Wetu, Simiyu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango nchini, TBS Dkt. Athuman Ngenya ameipongeza Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii kwa huduma bora kwa walengwa hasa wanawake na wananchi wa kipato cha chini.

Dkt. Ngenya ameyasema hayo katika Viwanja vya Nyakabindi, Simiyu baada ya kushuhudia huduma zinazotolewa na Wizara hiyo kwa walengwa.

Mkurugenzi huyo wa TBS ameeleza kuvutiwa huduma zinazotolewa na Wizara ili kuwawezesha walengwa hasa Wanawake na watu wenye hali ya chini.

“Nimevutiwa sana na huduma zenu kwa jamii mkishirikiana na TAMISEMI mtaweza kuwasaidia wajasriamali yakiwemo kuwawezesha kiuchumi" alisema.

Ameongeza kuwa TBS kwa upande wake ina inaendesha program maalum ya kuwawezesha wanawake kujiwezesha kiuchumi.
Afisa Ustawi wa Jamii Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Loata Mollel akitoa maelezo kwa mwananchi aliyetembelea banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya Nanenanekatika viwanja vya Nyakabindi, Simiyu.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango nchini, TBS Dkt.Athuman Ngenya (kulia) akiangalia majarida na vitabu mbalimbali vya miongozo inayotokewa na Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii wakati aipotembelea banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya Nanenanekatika viwanja vya Nyakabindi, Simiyu. Kushoto ni Afisa Ustawi wa Jamii Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Loata Mollel.

Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW