Header Ads Widget

UTAMBUZI WA KAYA MASKINI MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI TASAF WAANZA RASMI MANISPAA YA SHINYANGA



Mratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akizungumza katika kikao kazi kilichokutanisha pamoja Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya kutoa maelekezo namna ya kutambua kaya maskini zitakazoingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini TASAF III katika kipindi cha pili kilichoanza mwezi Juni mwaka huu 2020 katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna Manispaa ya Shinyanga leo Ijumaa Julai 3,2020 . Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akiwasisitiza Maafisa Watendaji wa Mitaa,vijiji na kata katika Manispaa ya Shinyanga kusimamia kwa uadilifu na umakini zoezi la utambuzi wa kaya maskini ambazo zitaingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini TASAF III katika kipindi cha pili ulionza mwezi Juni,2020. 
Mratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akiwasihi Maafisa Watendaji wa Mitaa,vijiji na kata katika Manispaa ya Shinyanga kusimamia kwa uadilifu na umakini zoezi la utambuzi wa kaya maskini ambazo zitaingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini TASAF III katika kipindi cha pili ulionza mwezi Juni,2020. 
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa katika kikao cha kuelezwa namna ya kutambua kaya maskini zitakazoingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini TASAF III katika kipindi cha pili. 
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone amewataka Maafisa Watendaji wa Mitaa,vijiji na kata katika Manispaa ya Shinyanga kusimamia kwa uadilifu na umakini zoezi la utambuzi wa kaya maskini ambazo zitaingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini TASAF III katika kipindi cha pili ulionza mwezi Juni,2020.



Kiwone ametoa rai hiyo leo Ijumaa Julai 3,2020 wakati wa kikao kazi kilichokutanisha pamoja Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya kutoa maelekezo namna ya kutambua kaya maskini zitakazoingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini TASAF III katika kipindi cha pili. 



Kiwone alisema utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini  katika kipindi cha pili umeanza mwezi Juni 2020 ambapo zoezi la utambuzi wa kaya maskini TASAF III katika Manispaa ya Shinyanga litafanyika kwa kipindi cha wiki mbili (kuanzia Julai 3 hadi Julai 20,2020). 


Alieleza kuwa zoezi la kutambua kaya maskini linalenga kaya maskini zilizosahaulika kwenye kipindi kilichopita lakini pia litahusisha mitaa na vijiji vyote katika Manispaa ya Shinyanga ambavyo havikuwepo kwenye mpango ambapo baada ya utambuzi huo wa awali ndipo serikali itajua inaenda kuhudumia walengwa wangapi na kutoa fedha kwa ajili ya kaya hizo.

 “Mpango huu wa kunusuru kaya maskini TASAF III kipindi cha pili utagusa kata zote na Manispaa ya Shinyanga. Tunawasihi sana viongozi kwenye maeneo husika wasimamie zoezi hili kwa umakini na uadilifu mkubwa ili tupate kaya ambazo zina vigezo na zinastahili kuwepo kwenye mpango”,alisema Kiwone.

“Hatutegemei kwenye eneo letu la Manispaa ya Shinyanga kupata kaya ambazo hazina sifa kuingia kwenye mpango. Kila mmoja atawajibika kwa nafasi yake kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni zilizowekwa lakini pia watu wasifanye kwa matashi yao",alisema Kiwone.

Alieleza kuwa ni haki ya kaya maskini kuhudumiwa siyo kwamba anapewa upendeleo ‘Favour’ au kwamba anapewa sadaka flani akibainisha kuwa hiyo ni fedha ya serikali inatakiwa iende kwa mtu stahiki na anayestahili kupata.

Hata hivyo alisema baada ya utambuzi huo wa awali kufanyika kuna vyombo vingine vyenye dhamana vitarudi kwenye orodha ya kaya maskini zinakazopatikana ili kuhakiki kama waliopitishwa ni kweli ni kaya maskini zina vigezo na zinastahili kuingia katika mpango wa kunusuru kaya maskini.

Alivitaja baadhi ya vigezo vinavyotakiwa katika mpango huo kuwa kaya zenye kipato duni zinazoshindwa kupata milo mitatu kwa siku,kaya yenye makazi duni, kaya yenye watoto wengi wanashindwa kuihudumia, kaya ambayo watoto wanashindwa kwenda shule kwa sababu hawana mahitaji ya shule au kwenda kliniki kwa sababu mbalimbali.

“Ni muda mzuri kwa wananchi pia kufahamu, wanapoitwa kwenye mikutano ya hadhara kwenye maeneo yao wafike ili wasikose haki yao ya msingi. 


Na kwa wananchi ‘makundi maalum’ ambao hawawezi kufika kwenye mikutano mfano watu wenye ulemavu,wazee maskini jamii iwataje. TASAF haiandikiwi mezani kupata orodha ya walengwa,orodha inapatikana kwenye mikutano ya hadhara,wakutambue kwamba wewe upo kwenye kaya maskini na mkutano uridhie kuwa kweli wewe ni kaya maskini”,alifafanua Kiwone.