` SHINYANGA WAADHIMISHA MIAKA 62 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR, KWA KUFANYA USAFI KUPANDA MITI

WANDAMAN HOTEL

SHINYANGA WAADHIMISHA MIAKA 62 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR, KWA KUFANYA USAFI KUPANDA MITI

 

SHINYANGA WAADHIMISHA MIAKA 62 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR, KWA KUFANYA USAFI KUPANDA MITI

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita, ameongoza maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwa kufanya usafi katika Hospitali ya wilaya ya Kishapu Jakaya Mrisho Kikwete, pamoja na kupanda miti katika shule ya awali na msingi Isoso.

Maadhimisho hayo ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, mkoani Shinyanga yamefanyika wilayani Kishapu, ikiwa ni sambamba na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya awali na msingi Isoso, pamoja na ushiriki wa michezo.
Mhita, akizungumza kwenye maadhimisho hayo, amewataka wananchi kuendelea kutunza mazingira, pamoja na kuepuka ukataji wa miti hovyo, ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, ambazo husababisha ukame hasa katika wilaya ya Kishapu.

Ndugu zangu hapa wilaya ya Kishapu, kama mnavyofahamu inakabiliwa na hali ya ukame, hivyo endeleeni kutunza mazingira na msikate miti hovyo, ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi,” amesema Mhita.
Aidha, akizungumza na wanafunzi wa shule ya Msingi na Sekondari Isoso, amewataka wasome kwa bidii ili kutimiza ndoto zao, sababu serikali chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuwaboreshea mazingira rafiki ya kusoma kwa ujenzi wa miundombinu mbalimbali.

Mhita, amewataka pia wananchi kuendelea kuuenzi na kuudumisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, pamoja na amani ya nchi.
Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Kishapu Mohamed Mkumbwa, amesema usafi katika Hospitali ikiwamo kufyeka majani, umesaidia kwa kiasi kikubwa klupunguza madhalia ya Mmbu, ili kukabiliana na ugonjwa wa Malaria.

Katika maadhimisho hayo,Mhita pia ametembelea wodi ya wazazi katika Hospitali ya wilaya ya Kishapu Jakaya Mrisho Kikwete, na kuwapatia zawadi mbalimbali wazazi.

VIDEO CHINI YA PICHA
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akipanda mti.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Peter Masindi akifyeka majani.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kishapu Emmanuel Johson akipanda mti.
TAZAMA VIDEO👇👇

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464