

Chuo cha
Biblia cha Philadelphia kinachomilikiwa na Kanisa la Philadelphia Miracle
Temple Kilichopo Kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga kimefanya mahafali yake
ya kwanza ya wahitimu wa ngazi ya Diploma na kuwataka kwenda kuihubiri injili
kwa ujasiri.
Akizungumza
kwenye mahafali Mgeni rasmi Mkuu wa chuo cha Calvary Reform Bible Institute Tanzania Lawrence
Daffa ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya kwanza Philadelphia Bible
College amesema elimu waliyopata ikawe chachu ya kuleta mabadiliko.
Amesema
wametumwa kwenda kwenye ulimwengu wa vita ya kiroho katika kunyenyua kusudi la
mungu na kupinga hila na upotevu wa ufalme wa giza,kwa kuwa dunia ya leo
inanjaa ya kiroho na imejaa mkanganyiko wa kimaadili na mara nyingi hupinga
ukweli wa neno la mungu.
Amesema ni
wakati wa kusimama kwa ujasiri Kupinga hila na upotevu wa ufalme wa giza ambapo
amesisitiza kuwa siyo wakati wa kurudi nyuma bali wakati wa kusimama kwa
ujasiri.
“Cheti
mnachopokea leo si karatasi tu bali ni agizo kutoka mbinguni la kuihubiri
injili kwa ujasiri,agizo la kuwasha nuru ya kristo katika giza la dunia
hii,agizo la kuishi kwa tofauti kama vyombo vitakatifu na vya haki mbele za binadamu na mungu”amesema Daffa.
Mkurugenzi wa chuo cha Philadelphia Bible College Askofu Baraka Laizer amesema lengo lao ifikapo mwaka 2030 kwa uwezo wa roho mtakatifu ni pamoja na kuwaendeleza kielimu baadhi ya wahitimu wa Diploma waliohitimu leo ili kupunguza tatizo la upungufu wa walimu.





Wageni waalikwa wakishuhudia matukio mbalimbali katika mahafari ya kwanza ya chuo cha Philadelphia











