Header Ads Widget

VIONGOZI WA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI NCHINI WAELEZA MAONYESHO YAMEWAPA CHACHU WAKUBALI KUBADILIKA KUJIKOMBOA

Moja ya banda la klabu ya waandishi wa habari yakikaguliwa na wajumbe wa bodi ya UTPC.

Na  Kareny Masasy,Dodoma

VIONGOZI  wa Klabu za waandishi wa habari   nchini wameeleza   kubadilika kuendana na kasi ya kidijitali  kutokana na  maonyesho ya mabanda kwa  mara ya kwanza  kufanyika  nakuonyesha namna  ya ufanyaji miradi na shughuli kwenye  maeneo yao kwa lengo la kuwakomboa waandishi.

Wakiongea kwa nyakati tofauti  jana tarehe 9,Desemba,2023 wakati wa maonyesho  viongozi hao  akiwemo mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari kutoka mkoani Shinyanga   Greyson Kakuru amesema  maonyesho hayo yamewapa chachu kwenda kuboresha zaidi   kwani wamekuwa wakipaza sauti  changamoto za kwenye jamii  kwa kushirikiana na wadau na serikali.

  Katibu wa  klabu ya waandishi wa habari  kutoka mkoani Ruvuma  Andrew Chatwanga  amesema  klabu zinasimamia vizuri majukumu ya waandishi wao na kujitahidi  kuwanyanyua .

Akitolea mfano kwenye klabu yake amesema  wameanzisha  kiwanda cha kukamua mafuta ya Alizeti ambacho kikianza kuzalisha waandishi watanufaika kwa kujinyanyua kiuchumi.

Mratibu wa  klabu ya waandishi wa habari Singida  Domiciana  Mwalusito amesema  maonyesho hayo amejifunza  kutoka kwenye mikoa mingine nini wamefanya  ili nao waweze kujiweka kwenye nafasi nzuri ya utekelezaji na kujinyanyua kiuchumi

“Tunaweza kuanzisha miradi  na kuajiri watu wengine bila kutegemea UTPC kwani klabu tayari ni taasisi hivyo viongozi wakiweka nia tunaweza”amesema  Mwalusito.

Mwekahazina wa klabu  ya waandishi wa habari kutoka mkoani Kagera  Alodia Dominick amesema  katika maonyesho haya amejifunza  kwani kuna miradi mingi yakufanya.

“Sisi tunaendelea kubuni  miradi tofauti tofauti  na tumeshawishika kurudisha gazeti letu la zamani lililokuwa likiitwa malengo yetu na waandishi wa habari watapata fursa kulitumia”amesema  Dominick.

Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari kutoka mkoani Mwanza Edwin Soko anasema  klabu zinafanya  za kijamii na zinaendelea kupaza sauti nakuonyesha kesho yake itakuwaje,utayari wa kujifunza  kutoka kwenye klabu zingine na kuwa na moyo wa kubadilika kwenda na dhana ya kutoka kwenye ubora na kuwa bora zaidi.

Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari  kutoka mkoa wa  Rukwa Nswima Ernest amesema  kwa mara ya kwanza waandishi wa habari wamekutana kwenye maonyesho kwa namna ya kujifunza  kuna masuala ya kijamii na kiuchumi.

“Zipo klabu ambazo zimejipanga vizuri zimeonyesha malengo yake na tumejifunza hakuna mtu yoyote wa kukupa raha,raha unajipa mwenyewe.”amesema Ernest.

Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari  kutoka mkoa wa Geita  Renatus Masuguliko amesema  maonyesho haya yameibua hali ya kuleta ushindani na kujipima  uwezo wake na mikakati waliyonayo ni kufikia malengo  kwa kuchochea na kuibua miradi.

Mwenyekiti wa  klabu ya waandishi wa habari kutoka mkoani Lindi Fatuma Maumba amesema  amejifunza kutoka kwenye klabu zingine na wakitoka hapa wanakwenda kuboresha  vya zamani na kuanzisha vitu vipya.

Mwekahazina kutoka klabu ya waandishi wa habari Zanzibar amesema Rahima Suleiman amesema  maonyesho haya  amejifunza kutoka kwenye klabu zingine  zinavyfanya kazi zipo zilizoanzisha vikoba na miradi ya pikipiki kwa kuona klabu zinaweza kuwasaidia wanachama kujikwamua kiuchumi



Makamu mwenyekiti wa UTPC  Pendo Mwakyembe akiweka saini kwenye moja ya banda la klabu ya waandishi wa habari  kwenye maonyesho ya mabada na shughuli wanazofanya

 Rais wa UTPC Deogratius Nsokolo  akiwa kwenye mabanda ya maonyesho yaliyoshirikisha klabu za waandishi wa habari mikoa yote 28

Post a Comment

0 Comments