Header Ads Widget

SHIRIKA LA POSTA LA PANDA MITI KWENYE CHANZO CHA MAJI MTO MUMBU KUTUNZA MAZINGIRA

Meneja wa Shirika la Posta Tanzania mkoani Shinyanga Julius Mponda (kushoto) akiwa na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi wakipanda miti kwenye chanzo cha maji mto mumbu ili kutunza mazingira.

Na Marco Maduhu,SHINYANGA

SHIRIKA la Posta Tanzania mkoani Shinyanga limepanda miti kwenye chanzo cha maji mto mumbu uliopo jirani na nyumba za Jeshi la Polisi maeneo ya Kambarage Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya kukilinda chanzo hicho na kutunza mazingira.

Zoezi hilo la upandaji miti limefanyika leo Februari 22, 2023, ambapo watumishi wa Shirika hilo la Posta walishirikiana na Askari Polisi kupanda miti kwenye chanzo hicho cha maji mto mumbu, na kupandwa jumla ya miti 150 ya matunda na kivuli.

Meneja wa Shirika la Posta Tanzania mkoani Shinyanga Julius Mponda, amesema wamepanda miti kwenye chanzo hicho cha maji ikiwa ni kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango alipokuwa mkoani Shinyanga aliagiza Taasisi za Serikali zishiriki kupanda miti kwenye vyanzo vya maji.

“Shirika la Posta Tanzania mkoani Shinyanga tupo hapa kupanda miti kwenye chanzo hiki cha maji mto mumbu, ili kutunza mazingira na pia kutekeleza agizo la Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango la Taasisi za Serikali kutunza mazingira nya vyanzo vya maji, na tumepanda miti 150 ya matunda na kivuli,”amesema Mponda.

Aidha, amesema miti ambayo wameipanda itasaidia kulinda chanzo hicho cha maji pamoja na kutunza mazingira kwa kuzuai momonyoko wa ardhi sababu mto huo upo jirani na makazi ya watu zikiwamo na nyumba za Jeshi la Polisi.

Katika hatua nyingine ametoa shukrani kwa Jeshi la Polisi, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na Manispaa kwa ushirikiano ambao wameutoa kwao na kufanikisha zoezi hilo la kupanda miti kwenye chanzo hicho cha maji mto mumbu.

Naye Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi, ambaye aliwaunga mkono Shirika hilo la Posta kupanda miti akiwa na Askari wake, amesema miti hiyo wataitunza ikue, huku akitoa wito kwa wananchi wa Shinyanga, wapande miti kwa wingi sababu miti ni uhai na inatunza mazingira.

Amesema miti mingi ikipandwa kila mahali itaifanya Shinyanga kuwa ya kijana pamoja na kumaliza tatizo la ukame.

Meneja wa Shirika la Posta Tanzania mkoani Shinyanga Julius Mponda akizungumza kwenye zoezi hilo la upandaji miti.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi akizungumza kwenye zoezi hilo la upandaji miti.

Meneja wa Shirika la Posta Tanzania mkoani Shinyanga Julius Mponda akipanda mti.

Meneja wa Shirika la Posta Tanzania mkoani Shinyanga Julius Mponda akipanda mti.

Meneja wa Shirika la Posta Tanzania mkoani Shinyanga Julius Mponda akipanda mti.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi akipanda mti.

Afisa Maliasili na Mazingira Manispaa ya Shinyanga Ezra Manjerenga akipanda Mti.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.
Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Awali Picha ya pamoja ikipigwa kwenye zoezi hilo la upandaji miti kabla ya kupandwa kwenye chanzo cha maji mto mumbu.

Awali Picha ya pamoja ikipigwa kwenye zoezi hilo la upandaji miti kabla ya kupandwa kwenye chanzo cha maji mto mumbu.

Awali Picha ya pamoja ikipigwa kwenye zoezi hilo la upandaji miti kabla ya kupandwa kwenye chanzo cha maji mto mumbu.

Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania mkoani Shinyanga wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumaliza kupanda miti kwenye chanzo cha maji mto mumbu.

Picha ya pamoja ikipigwa.

Post a Comment

0 Comments