Header Ads Widget

HUDUMA ZA UTOAJI HATI YA ADRHI WILAYANI KAHAMA ZIMEANZA




Msajili msaidizi wa hati   mkoani Shinyanga Emanuel Gwaltu  akiwa katika zoezi la utoaji wa hati  kwa wananchi  wilayani Kahama. 

Na  Kareny  Masasy ,Kahama

KAMISHNA  wa  ardhi  msaidizi mkoani Shinyanga Leo Komba  amesema  zoezi la  ugawaji wa hati  500 kwa wananchi wilayani Kahama  kupitia kliniki tembezi ya utoaji na ugawaji  hati kwa wamiliki wa viwanja  walioomba limeanzia  wilayni humo.

Akizungumza  leo tarehe 17/11/2022  kwenye eneo la shunu  kata ya Nyahanga ambalo  lina mradi wa ugawaji wa viwanja kamshina  Komba amesema   wananchi walio wengi  bado hawana muamko wa kushughulikia hati za umiliki wa viwanja vyao.

Kamishna Komba amesema wameamua kutoa huduma  hiyo kwa ukaribu  nakuwataka wenye viwanja vilivyopimwa tayari waje na nyaraka zao  watahudumiwa na kupata hati..

“Tumeanzia wilaya ya Kahama na tunafanya kazi hii muda wa siku mbili na tukimaliza tunahamia wilaya zingine tunataka kazi hii iwe endelevu”amesema Komba.

Msajili wa hati msaidizi  kutoka mkoani Shinyanga  Emanuel Gwaltu amesema   wamekuja kugawa hati  ambazo ziko tayari  na zimesajiliwa  nakuwaeleza wananchi faida ya kumiliki hati ya viwanja ni kupata mkopo kwenye taasisi ya fedha  na kujinyanyua kiuchumi.

“Ninacho washauri wananchi wazitunze hati zao vizuri  zitawasaidia katika masuala mengi pia walio na viwanja wavisajili viwanja vyao kwa kupata hati miliki ya kudumu”amesema  Gwaltu.

Japheti Kaliua  na   Hawa said wamesema  wamefuatilia hati zao kwa muda mrefu lakini sasa zoezi walilolianzisha kuwafuata wananchi  litaondoa urasimu wa kuzungushwa kwa kupigwa tarehe hivyo wamefurahi.



Maafisa ardhi wakiwa katika viwanja vya ofisi ya mtaa wa Shunu wilayani Kahama wakitoa hati kwa wananchi waliokuwa wameomba.

watumishi wa ofisi ya ardhi mkoa wa Shinyanga wakijiandaa na kazi 

Kamishna msaidizi wa ardhi  kutoka mkoani Shinyanga Leo Komba akiwa  kwenye zoezi la ugawaji wa hati kwa wananchi wilayani Kahama.




Kamishna msaidizi wa ardhi  kutoka mkoani Shinyanga Leo Komba akiwa  kwenye zoezi la ugawaji wa hati kwa wananchi wilayani Kahama.



Post a Comment

0 Comments