Header Ads Widget

TCRA, UCSAF WASISITIZA WATOA HUDUMA ZA MAWASILIANO 'RADIO & TV' KUJENGA MINARA YA PAMOJA


Mkuu wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya UCSAF akiwahamasisha watoa huduma za mawasiliano kuungana kuomba ruzuku kujenga minara ili kuongeza usikivu wa vyombo vyao vya habari kwenye maeneo yasiyosikika. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Fedha na Utawala UCSAF, Pius Joseph.  Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Idara ya Uendeshaji UCSAF, Albert Richard akifuatiwa na Kaimu Katibu wa UCSAF ,Ipyana Jengela.

Na Kadama Malunde - Mwanza

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) umekutana na wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwemo wamiliki wa vituo vya Radio, Televisheni, watoa huduma za usafirishaji wa vifurushi na watoa huduma ya maudhui mtandaoni kwa lengo la kuwajengea uelewa watoa huduma na wadau hao kushiriki shughuli za mfuko wa UCSAF na kutimiza wajibu wao kisheria. 

Akizungumza katika Mkutano huo leo Agosti,31 2020 uliofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Idara ya Fedha na Utawala UCSAF, Pius Joseph alisema mkutano ulilenga kuwajengea uelewa wadau wa mawasiliano namna mfuko wa UCSAF unavyofanya kazi na wajibu wao kisheria.

Joseph aliyataja miongoni mwa mafanikio yaliyofikiwa na mfuko wa UCSAF ni pamoja na kufikisha huduma ya mawasiliano ya simu katika kata 631 kati ya kata 994 zilizosainiwa mkataba,ufikishwaji wa matangazo ya runinga ya kidigitali katika mikoa ya Katavi, Geita,Simiyu,Njombe na Songwe pamoja na ujenzi wa vituo 10 vya TEHAMA Zanzibar na 11 Tanzania bara ambapo kituo kimoja kimejengwa katika kila wilaya. 

Hata hivyo alisema suala la ucheleweshaji wa utekelezaji wa miradi unaathiri kasi ya mfuko kufikisha mawasiliano,ukosefu wa fedha za kutosha kufikisha mawasiliano kwa kipindi kifupi zaidi kulingana na mahitaji na uelewa wa watoa huduma na wadau mbalimbali kushiriki shughuli za mfuko na kutimiza wajibu wao kisheria. 

Joseph aliwashauri wamiliki wa vituo vya utangazaji kushirikiana kujenga minara ya pamoja ili kupunguza gharama za kuendesha vituo vya matangazo na kwamba UCSAF inachofanya ni kuwawezesha watoa huduma kwa kuwapa ruzuku ili kujenga minara. 

Kwa upande wake, Mkuu wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya UCSAF alisema upenyo wa kuenea kwa vyombo vya habari kanda ya Ziwa bado hauridhishi ambapo usikivu wa redio Kanda ya Ziwa upo chini ya asilimia 50 hivyo kuwaomba Watoa huduma za mawasiliano kuomba Ruzuku UCSAF kwa ajili ya kujenga minara ya pamoja ili walau usikivu ufikia asilimia 60. 

“Mkijenga minara maeneo mengine,kama kuna mnara umejengwa na wadau wa sekta ya utangazaji,gharama zitapungua. Tuache ubinafsi tutumie minara iliyojengwa kwa ruzuku ya serikali. Lengo tunataka kuongeza usikivu wa radio Kanda ya Ziwa”,alisema Mhandisi Mihayo. 

"Kuna watu wanawafanya nyinyi kama vitega uchumi, akili kubwa mnaelekeza kulipia kodi ya minara ili msizimiwe matangazo,hao wanaowapangisha silaha yao kubwa ni kuzima matangazo. Nawasihi wamiliki wa vituo vya utangazaji kuungana. 

Tumieni nafasi hii mji – organize, leteni maombi UCSAF kujenga mnara wa pamoja ili kupunguza gharama za uendeshaji wa vituo vyenu tuache wivu na ubinafsi. Jengeni na kumiliki vya kwenu kupitia ruzuku ya serikali, tunataka mjenge wote, utakachotakiwa kufanya ni utachangia umeme na kulipa mlinzi tu”,aliongeza Mihayo. 

Hata hivyo Mjumbe wa Bodi ya UCSAF, Samweli Nyalla  alisema lengo la UCSAF kuhamasisha watoa huduma za mawasiliano kujenga minara ya pamoja ni kutaka kupeleka matangazo sehemu ambazo hakuna mawasiliano.

"Sasa hatuangalii pale ulipo,tunaangalia kule ambako hufiki,kule unapotakiwa kupeleka mawasiliano ili kuboresha zaidi huduma za mawasiliano",alisema Nyalla. 

Miongoni mwa maazimio yaliyofikiwa na washiriki wa mkutano huo ni pamoja na kulipa tozo kwa mujibu wa sheria,maombi ya mnara kwenye maeneo husika ufanywe na watoa huduma za radio na TV kupitia wawakilishi waliopo katika mkoa husika na mnara unapoanzishwa utumike kwa watoa huduma watakaohitaji kwa kulipia ghrama za umeme na ulinzi na UCSAF ujikite kutoa elimu ya mfuko na wajibu wa watoa huduma za mawasiliano.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI

Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) akizungumza wakati akifungua Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwemo wamiliki wa vituo vya Radio, Televisheni, watoa huduma za usafirishaji wa vifurushi na watoa huduma ya maudhui mtandaoni ulioandaliwa na TCRA kwa kushirikiana na UCSAF uliofanyika leo Agosti 31,2020  katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza . Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) akizungumza katika Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa.
Mkuu wa Idara ya Fedha na Utawala UCSAF, Pius Joseph akielezea kuhusu mafanikio mbalimbali yaliyofikiwa na UCSAF. 
Kaimu Katibu wa UCSAF ,Ipyana Jengela akitoa mada kuhusu uanzishwaji wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote na malengo ya mfuko huo.
Mkuu wa Idara ya Uendeshaji UCSAF, Albert Richard akielezea kuhusu miradi mbalimbali inayotekelezwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF).
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwemo wamiliki wa vituo vya Radio, Televisheni, watoa huduma za usafirishaji wa vifurushi na watoa huduma ya maudhui mtandaoni wakiwa kwenye kikao kilichoandaliwa na TCRA na UCSAF.
Mjumbe wa Bodi ya UCSAF, Samweli Nyalla akizungumza katika mkutano huo.
Mkuu wa Idara ya Fedha na Utawala UCSAF, Pius Joseph akizungumza ukumbini.
 Mkurugenzi wa Malunde Media 'Malunde 1 blog', Kadama Malunde akiwa ukumbini.
Mkurugenzi wa Malunde Media 'Malunde 1 blog' , Kadama Malunde (kulia) na Estomine Henry kutoka Shinyanga Press Club blog wakiwa ukumbini.
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwemo wamiliki wa vituo vya Radio, Televisheni, watoa huduma za usafirishaji wa vifurushi na watoa huduma ya maudhui mtandaoni wakiwa kwenye kikao kilichoandaliwa na TCRA na UCSAF.
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakisoma vipeperushi vya UCSAF.
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakisoma vipeperushi vya UCSAF.
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakisoma vipeperushi vya UCSAF.
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakisoma vipeperushi vya UCSAF.
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini

Mdau wa Mawasiliano Emmanuel Msigwa kutoka Victoria FM akiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Maafisa wa TCRA Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini


Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog