Header Ads Widget

MAFUNZO YA WANAHABARI KUANDIKA HABARI ZA UHURU WA KUJIELEZA YAHITIMISHWA MKOANI SINGIDA

Wanahabari wakiwa kwenye mafunzo ya kuandika habari za uhuru wa kujieleza.

Na Marco Maduhu, SINGIDA

MAFUNZO ya kuandika habari za uhuru wa kujieleza kwa Wanahabari wapatao 40 kutoka Mikoa ya Tabora, Dodoma, Shinyanga, Simiyu na Singida yamehitimishwa Rasmi.

Mafunzo hayo yalianza kutolewa Novemba 3, 2022 yamehitimishwa leo Novemba 5, ambayo yalikuwa yakiratibiwa na Taasisi ya vyombo vya habari kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (Misa-Tan)kwa ufadhili wa Ubalozi wa Kanada nchini Tanzania.

Mwezeshaji wa Mafunzo hayo Marko Gideon, amesema Wanahabari wanapaswa kutumia kalamu zao vyema kuandika habari za uhuru wa kujieleza katika Nyanja mbalimbali na kupaza sauti za wananchi.

Amesema unapokosekana uhuru wa kujieleza, Utawala wa kisheria hautakuwepo, uwajibikaji kwa viongozi, hakutakuwa na usawa wa kisheria, hakuna uwazi, uchaguzi hauwezi kuwa huru na haki, wala kudhibiti matumizi mabaya ya viongozi, " amesema Gideon.

Naye Andrew Marawiti kutoka Misa-Tan, amesema baada ya mafunzo hayo wanatarajia kuona Wanahabari wakiandika habari nyingi zinazohusu uhuru wa kujieleza.

Nao baadhi ya Wanahabari walioshiriki mafunzo hayo, wamesema mafunzo hayo yamewaongezea ujuzi na weledi wakati wa utekelezaji wa majukumu yao kwa kuandika habari za uhuru wa kujieleza pamoja na kuzingatia usawa wa kijinsia kwa vyanzo vyao vya habari.

Mwezeshaji Marko Gideoni akitoa mafunzo ya uhuru wa kujieleza kwa Wanahabari.

Mwanahabari Amini Nyaungo kutoka Radio Standard FM mkoani Singida akichangia mada kwenye mafunzo hayo.

Mwanahabari Jeniva kutoka Radio Faraja mkoani Shinyanga akichangia mada kwenye mafunzo hayo.

Wanahabari wakiendelea na mafunzo.

Wanahabari wakiendelea na mafunzo.

Wanahabari wakiwa kwenye mafunzo.

Wanahabari wakiwa kwenye mafunzo.

Wanahabari wakiwa kwenye mafunzo ya vitendo katika kazi za makundi.

Wanahabari wakiwa kwenye mafunzo ya vitendo katika kazi za makundi.
Picha ya pamoja ikipigwa mara baada ya mafunzo kumalizika

Post a Comment

0 Comments